Thursday, June 14, 2012

Anzisha mradi

Wapo wengi walioajiriwa wanatamani kuanzisha mradi huku wakiendelea kuwa kazini, na kwa kuwa hawawezi kuacha kazi wanaishia kununua bodaboda, bajaj, au taxi... At the end of the day wanaishia kugombana na madereva

Guys mradi wowote unahitaji capital na muda wa ufatiliaji la sivyo utatwanga maji kwenye kinu

Kama capital unayo fungua duka food staffs, kama mtaji wako mzuri zaidi waweza fungua mini supermarket, lakini sio uswahilini coz biashara za huko ni Za maduta ya taa na sembe huwezi icontrol ukiwa kazini

Waweza pia anzisha biashara ya diesel kama una capital ya @least 15000$, inalipa vizuri kama laki mbili kwa siku wakati biashara inaanza, ukichangamka inalipa vizuri saaaaaaana

Nnavyosikia sikia uwakala wa Mpesa na Tigo pesa pia unalipa pia. 5mil Capital can make difference

Biashara ya kununua gari japan kwa kulipia online then ikija hapa utauza au kununua ili uuze na wewe upo kazini full time itakula kwako

Ushawahi fikiria biashara ya packaging? Kwa mfano unasajili jina, then unakuwa na brand yako ya sukari ya mfuko wa kilo moja unasupply kwenye supermarkets... Capital ya 7mil inatosha

Salon za kike na za kiume pia sinalipa bt sijawahi fanya hio biashara

Wale ndugu zangu wa mbeya wanajua ule mpango wa kununua mchele wakati wa msimu na kuuza wakati wa kiangazi.. Inalipa pia kama hutaki chakarika saaana..

Zipo biashara nyingi kwa wenye capital, kana capital yako ndogo, acha kazi ukuze mtaji.. Nitafunguka zaidi nikipata muda

No comments:

Post a Comment