Thursday, June 28, 2012

LA ULIMBOKA LIWE FUNZO

Hakuna hata mtanzania mmoja ambaye anaweza furahishwa na jambo lililomkuta DR ulimboka, tumuombee mungu amponeshe kwa haraka aendelee simamia lile ambalo yeye anaona ni sahihi

Lakini kubwa zaidi lililonitia hamasa ya kuandika ni wepesi wetu watanzania wa kuhukumu, tunawaachia watoto zetu urithi mbaya sana

Nisieleweke kuwa napingana na kile mnachoamini ninyi bali najaribu kwenda zaidi ya imani yenu.

Vipi Mheshimiwa LEMA angefariki kwa kifo cha kawaida tu kama binadamu wengine ambavyo hufa siku ya pili baada ya kumuandikia waraka rais kikwete? Kwa style yetu ya kuhukumu tungekuwa na amani sisi?

Au Vipi kama mimi nakitaka kiti cha mnyika cha Ubunge na hivyo baada ya drama za "rais dhaifu" nikaamua kumvizia na kumdhuru, nani atanihisi? Najua mtakuwa mshamtaja mhusika bila kunihusisha kabisaaa

Naogopa sana kugusia imani ya wengi juu ya kifo cha sokoine na amina chifupa kwa kuwa itanilazimu niamini na kifo cha chacha wangwe

Nilijaribu soma btn the lines chanzo na matukio ya Rwanda genocide na uhusika wa Ufaransa na kagame, halafu nikasoma utawala wa SIAD BARRE wa somalia, utawala wake, kifo chake na somalia ya leo.

Ikulu ni mahali patamu sana, na wanasiasa wana mbinu nyingi sana za kubaki madarakani au kuingia madarakani Ikibidi hata kwa damu, KENYA ni mfano mzuri... TUJIANGALIE TUNAWEZA GONGANISHWA VICHWA KWA USHAHIDI WA KIMAZINGIRA

Lakini swali la msingi, hawa waliomteka dr ulimboka naskia walikua na bunduki, wamezipata wapi? Kama serikali ingeweka ulinzi wa kutosha tusingeihusisha kirahisi katika mambo kama haya, they should play their part or else kila siku tutaihusisha na kila jambo baya

Anyways ni maoni yangu tu ila mtaani kwetu ukimwambia mtu utanikoma wewe siku ya pili akidhurika polisi wanakubeba, zamu yetu sasa na sisi kuamini kama ambavyo wao huamini yale ya mtaani kwetu

Friday, June 22, 2012

MNYIKA HAKUKOSEA

Mara ya kwanza niliona mnyika amekosea sana kumwita rais Dhaifu, hii ni kutokana na ukweli kuwa kanuni za bunge hazimruhusu, lakini pia ameyasema yale mbele ya watanzania wote ambao wapo wenye mapenzi thabit kwa rais. Lakini kumbe rais amemruhusu mnyika aseme maneno yale

Hivi ni nani hajawahi ona watoto wa darasa la kwanza wanafunga barabara kwa kuwa mwenzao amegongwa mpaka matuta yawekwe, na siku hiyo hiyo matuta yanawekwa? Tumemfundisha nini mtoto huyu? Tumemfundisha serikali yako ni dhaifu lakini ukiishikia kiboko inatekeleza hapo hapo

Wakati wa mkapa wanafunzi udsm waligoma, mkapa akafunga chuo mwaka mzima, hatukusikia tena mgomo mpaka 2007 wakati wa kikwete, tuliposikilizwa tulichogomea, tuligoma kwa kila kitu hata kama hatukustahili

Kitendo cha mtu kusimama mbele ya bunge akapata courage ya kusema rais dhaifu, akarudia na kurudia peke yake inaprove kama rais ni dhaifu

USHAURI WA BURE KWA RAIS:
Haiwezekani sovereign country tunaambiwa kuna muwekezaji ana passport tano, serikali imemshindwa, KWELI? Serikali ya watu mil 40, jeshi, police, na TISS, inaandikwa gazetini imemshindwa mtu mmoja? Vaa mkono wa chuma baba

Hakuna uhuru usio na mipaka mheshimiwa kikwete. He who wishes to be obeyed must know how to command, uhuru ukizidi sana tunaharibu nchi. Unatuachia saaaana mpaka tunaanza kukukosea heshima

Madaktari wamegoma, tukaambiwa rudini kazini haraka au tutawafukuza wote tutaleta wanajeshi wafanye kazi, then kesho tunawaita tunakaa nao mezani, baba watakupanda kichwani washajua una udhaifu, unawaogopa..

Machiavelli anasema If an injury has to be done to a man it should be so severe that his vengeance need not be feared..

Kwa mfano watoto wanagoma lazma matuta yawekwe, waagize walimu wao wawatandike viboko watoto warudi darasani, then baada ya mwezi weka tuta kuzuia ajali kwa kuwa hapo mwanzo walikaa miaka bila tu.

Tunagomagoma kila kitu kwa sababu unaturuhusu, lakini pia haujali.. Wanafunzi wagome, madokta wagome, walimu wagome, hivi nani anawapa kiburi? Hawa madokta nani anawapa kiburi cha kugomea serikali?

Men are so simple and so much inclined to obey immediate needs that a deceiver will never lack victims for his deceptions.
Sent from my BlackBerry® smartphone on the Tigo Tanzania Network

Thursday, June 14, 2012

Anzisha mradi

Wapo wengi walioajiriwa wanatamani kuanzisha mradi huku wakiendelea kuwa kazini, na kwa kuwa hawawezi kuacha kazi wanaishia kununua bodaboda, bajaj, au taxi... At the end of the day wanaishia kugombana na madereva

Guys mradi wowote unahitaji capital na muda wa ufatiliaji la sivyo utatwanga maji kwenye kinu

Kama capital unayo fungua duka food staffs, kama mtaji wako mzuri zaidi waweza fungua mini supermarket, lakini sio uswahilini coz biashara za huko ni Za maduta ya taa na sembe huwezi icontrol ukiwa kazini

Waweza pia anzisha biashara ya diesel kama una capital ya @least 15000$, inalipa vizuri kama laki mbili kwa siku wakati biashara inaanza, ukichangamka inalipa vizuri saaaaaaana

Nnavyosikia sikia uwakala wa Mpesa na Tigo pesa pia unalipa pia. 5mil Capital can make difference

Biashara ya kununua gari japan kwa kulipia online then ikija hapa utauza au kununua ili uuze na wewe upo kazini full time itakula kwako

Ushawahi fikiria biashara ya packaging? Kwa mfano unasajili jina, then unakuwa na brand yako ya sukari ya mfuko wa kilo moja unasupply kwenye supermarkets... Capital ya 7mil inatosha

Salon za kike na za kiume pia sinalipa bt sijawahi fanya hio biashara

Wale ndugu zangu wa mbeya wanajua ule mpango wa kununua mchele wakati wa msimu na kuuza wakati wa kiangazi.. Inalipa pia kama hutaki chakarika saaana..

Zipo biashara nyingi kwa wenye capital, kana capital yako ndogo, acha kazi ukuze mtaji.. Nitafunguka zaidi nikipata muda

Tuesday, June 5, 2012

TUMETOA DODOKI, TUMEWEKA JIWE LA KUSUGULIA MIGUU

Wakati wa bunge la budget mwaka 2011, mheshimiwa kafulila alimtuhumu Bw Zambi na mbunge mwenzie Omary badwel kwa kuomba rushwa wanapoenda kufanya kazi, akaamriwa kukaa chini

Mheshimiwa felix mkosamali akasimama kuomba muongozo wa mwenyekiti wa bunge ambaye alikuwa mh Simbachawene kwa kuwa tuhuma ni nzito kwa mbunge kuambiwa kaomba rushwa mbele ya bunge tukufu

Mh Simbachawene akasema atalitolea maelezo lakini mpaka leo akalipotezea na hakusema chochote

Leo hii, badwel, mwaka mmoja baadae anakamatwa kwa kosa lile lile la kuomba Rushwa na kufikishwa mahakamani na bw Simbachawene leo hii kapandishwa na kuwa naibu waziri wa nishati na madini.. Usishangae siku akipewa uwaziri kamili wizara hiyo. Wizara yenye kashfa za kutosha..

Monday, June 4, 2012

KATIBA NIITAKAYO

1. SYSTEM OF ELECTION IBADILIKE
hapa Tanzania tumezoa first past the post FPTP ambayo anayeongoza kwa kura anachukua madaraka. kwa mtazamo wangu system hii ya uchaguzi ndiyo inayotufanya tushindwe kupiga kura kwa upande mmoja lakini kwa upande wa pili, inasababisha upotevu wa kura nyingi. kwa mfano Rais Kikwete anaongoza nchi kwa kupata kura 5,276,827 ambayo ukigawanya kwa watanzania miloni 40 ni sawa na aslimia 12.5 ya watanzania wote

lakini pili Dr slaa alipata kura 2,271,941 ambazo ni karibia nusu ya kura Za kikwete, hii  ni kusema zaidi ya watu milioni mbili maoni yao hayajasikilizwa. haiwezekekani watanzania zaidi ya milioni mbili wamchague mtu halafu maoni yao yapotee kwa kuwa wamezidiwa na wengine, kesho hawatapiga kura

katiba mpya ilete system ya propotional Representative ambayo uwakilishi serikalini utatokana na idadi ya asilimia katika kura zilizopigwa. Kwa system hii, hakuna kura itakayopotea kwa maana, hata group dogo la watu kura zao zitapata muwakilishi kwenye serikali hivyo watanzania wataamka kupiga kura

2. MFUMO WA SERIKALI 3
So far tuna mfumo wa serikali mbili, serikali kuu na SMZ, haya ni mapungufu. Zanzibar imeungana na maiti? Tanganyika irudi iwe na serikali yake, Zanzibar iwe na serikali yake na kuwe na serikali kuu ya Tanzania ambayo itakuwa na Rais, makamu, waziri wa ulinzi, mambo ya nje na fedha tu. hii itakata mzizi wa fitina.

3. RAIS ASISHITAKIWE LAKINI, ALIPE MSHAHARA NA POSHO ALIYOPEWA KAMA HAKUTIMIZA AHADI
najua hii itasound kama kichekesho lakini ilani ya uchaguzi ya mgombea husika ni kama business plan, wananchi wanamchagua mgombea flani kutokana na ilani yake, je kama hakutimiza yale aliyosema atafanya, vipi aondoke na mshahara ambao sisi tumempa kwa kazi ambayo hajaifanya.

tumemuona Obama anahaha kuconvince congress lipitishe mambo yaliyo kwenye ilani yake mfano ahadi juu ya bima ya afya, kwa kuwa hiyo ilani ndio iliyompa uongozi

4. JESHI LA WANANCHI NA MAGEREZA YAWE SEHEMU YA KIJAMII NA 25% YA BUDGET YAKE INJITEGEMEE
tufute leseni zote za wakandarasi kutoka nje na kazi za ujenzi wa barabara na kandarasi kubwa ziende kwa jeshi la wananchi. m not suggesting kuwa jeshi halina kazi, lakini lina human resources nyingi za kuweza kufanya kazi za kandarasi na pesa ya ujenzi ikalipe mishahara. natambua kama JKT wanajitahidi kupitia SUMA JKT lakini JWTZ ndio linaloweza zaidi.

kule south Africa wamepiga marufuku gari za kijapan kutembea kwenye ardhi yao labda kwa kibali maalum tangu walivyoamua kutengeneza magari. tuna jeshi lenye watu shupavu, tuna amani, kwa nini mkandarasi wa barabara ya mwenge ubungo awe mchina????

mwengine kaiba kuku wa 15,000 kafungwa miezi sita katumia chakula cha sh 270'000. kwa nini asiambiwe wewe, na wewe, na wewe, mmehukumiwa kupalilia pamba hii mpaka mavuno

5. SHERIA YA KUMLINDA MLAJI
ukinunua gazeti limeandika habari ya uwongo unaruhusiwa kulishtaki na unalipwa fidia, kampuni ya simu imetangaza shilingi kwa sekunde, ikipandisha bei itangaze au ikikata kinyemela ishitakiwe

6. Waziri asiwe mbunge
7. barabara ikitaka kupita kwenye eneo la makazi ya watu, wasilipwe fidia bali serikali ile gharama stahiki za kununua nyumba eneo lile
8. mwananchi ndio mwenye nchi

Friday, June 1, 2012

PRICELESS MEMORIES

nilipoamka asubuhi daaaaaah baridi sana na mama ananilazimisha kuoga. nikaoga chap chap, nikavaa bukta yangu ya blue, shati jeupe, kidumu na  ufagio mkono wa kushoto, nishapakwa mafuta ya AYUU chap chap.. kwa kuwa kipindi kile sikuwa na saa so sikujua kama nimewahi au nimechelewa shule, kutoka nje watoto wenzangu nao wapo njiani kwenda shule.

mara tukapita sehemu yenye redio, haa kumbe ndio kwanza kipindi cha majira kinaanza, hii itakuwa saa 12 na nusu, tukaanza kucheza njiani, tunaenda shule huku "tunabaka' panzi. kufika shule tumewahi, bbada ya kuhesabiwa namba mstarini wanafunzi wakaambiwa wakafagie, sisi darasa la kwanza tukaanza kucheza makida makida. tunaimba *makiiida makiiiiida makida nzeeee* yeeeeee

ah muda wa darasani si ukafika. tukaanza soma hiiii ndio oooooo, o,o,o, ipo kama yaaaaai o,o,o,oooo. na hii ndio uuuuuuu, u u uu, ipo kama kikoooombeeee u,u,u. kwa kipindi kile sikujua how fun it was leo ndio naona raha yake.

hivi ni shule yetu tu au na nyie mlikuwa mnasema ELOMENO PIIII KYU mkifikia zile alphabets za L  M N O P Q ?? hivi ni dunia nzima? na hii W mlikuwa "mnasema double U" mbona imekaa kama "double V"

anyways kengele ikagongwa tulishangiliajeeeeee. kutoka nje najiuliza, hii sh 5 ya kutumia niliyopewa ninunue gudi gudi, au nikanunue mihogo? ah bora nile ashkirimu kwa bibi kibo anauza ashkirimu za maziwa.

sisi tuliotoka shule saa tano tulikuwa na raha, kaka huko darasani kwao ndio kwanza wanasoma kitabu cha darasa la tano, naskia wanasoma "siku ya gulio Katerero" ile ya jana chopeko na mnofu au hadithi ya juma na rosa kama sikosei watakuwa washamaliza kuisoma

basi sisi tukaondoka kulelekea nyumbani huku tunacheza kitenesi ayyyyaaaa mvua ikaanza kunyesha, raha ilioje, nikavua viatu nikaweka kwenye begi nikaaza safari na mvua, meno ya juu yanagonga ya chini kwa baridi, kufika njia ya kanisani, lile kanisa lina paa kuuuuuubwa hivyo maji ya mvua yanatiririka kwa wingi, tukajitega chini ya paa, daaah hiyo mvua inavyotuangukia sasa. barrrriiiidddiiiiiiiii

nyumbani sasa, mama ananiambia baridi inatia homa so nikachange chap chap, nikala kiporo cha ubwabwa na maharage huyoooooo  nikaenda angua maembe kwa mzee juma. kumbe kaka angu wana safari ya kishule kutembelea makumbusho ya taifa, wakapita pale nyumbani kwenye gari wamejaaa na walimu wao wanaimba kwa sauti kubwaaa  "dereeeeva tubwageeee, dereeeva ongeza mwendoooooo" wana raha, na mimi nikiwa darasa la tano nitaimba kwenye gari

any ways jioni hii mama kanikataza kuwinda ndege, so navaa manati yangu shingoni narudi nyumbani taratiiiiibu huku navizia jirani naona usiku wanapika ubwabwa. hakuna kitu homework na  sina haja ya kuwahi kulala leo kwa kuwa kesho ni jumamosi, jambo la muhimu kesho ni kipindi cha mama na mwana muendelezo wa hadithi ya binti chaupele na msimulizi HALIMA KIHEMBA

ah yamepita hayo, mimi leo hii ni waziri, rais, mbunge, muajiriwa, mtu mzima, mheshimiwa na nimewasahau wale wote nilioimba nao ukuti, na nafasi yangu niliyonayo sasa imenitia upofu kabisa juu ya watoto na haki zao, viwanja vyao (open space) tunavidhulumu, walimu hatuwalipi tena mishahara, watoto wa kike ninawatumikisha nyumbani kwangu, watoto wa kiume tumeshawapa ajira ya kuokota vyuma na sina mpango wowote wa kuwasaidia watoto wafurahie utoto wao kama nilivyofurahia mimi... #changeTanzania

#ZANZIBAR REVEALED

 kuna dhana ya kuwa karume aliuawa kulinda muungano, mazingira yote ya kuuawa kwa karume haiihusishi tanganyika kwa namna moja ama nyengine katika mauaji hayo na kwamba ni wananchi walichoshwa na serikali yao. kinachotokea leo zanzibar, ni msingi mbovu wa utawala wa tokea awali na kamwe tanganyika isihusishwe. 

jarida moja la kila mwezi 'Africa Events' la Agosti 1992 (uk. 27) ,linadai sababu za kuuawa kwa Karume zilikuwa za kibinafsi kwa njia ya kulipa kisasi. Inaelezwa kwamba Muhammed Hamud, mtoto wa Hamud Muhammed Hamud, aliyetiwa kizuizini miezi michache baa­da ya mapinduzi ya 1964 akituhumiwa kutaka kuipindua Serikali ya Karume.
Miaka, rnichache baadaye, Luteni Hamud Muhammed Hamud akiwa katika mafunzo ya kijeshi huko Tashkent (Urusi ya zamani), aliambiwa na mwanafun­zi mwenzake kwamba mzee Hamud alinyongwa na Karume akiwa kizuizini hila kufunguliwa mashtaka. Kwa taarifa hiyo, Luteni Hamud alisikika akiapa ange­muua Karume akirejea Zanzibar.
Taarifa ya kusudio la Hamud la kuua ilifikishwa kwa vyombo vya usalama Visiwani na wenzake, lakini hakukamatwa wala kuwekwa wa chini ya uchunguzi mkali ali­porejea Zanzibar; badala yake ali­pandishwa cheo kuwa luteni na Karume mwenyewe.
Jarida hili halisemi lolote juu ya raja Ali Khatibu Chwaya na ko­plo mwingine juu ya kushiriki kwao katika mauaji haya. Hata hivyo,. Kushiriki kwao kunaelekea kutetea dhana ya pili kwamba kwa sababu Serikali Karume ilishindwa kukidhi matarajio ya Wazanzibari wengi, hapakuwa na njia mbadala ila kumwondoa Karume ili kuleta mabadiliko.

Hapa panazuka swali; kama lengo la Hamud la kumuua Karume lilikuwa kulipa kisasi, kwa nini tukio hili lilihusisha watu zaidi ya mmoja? Si hivyo tu; kwa nini watu zaidi ya 1,000 walikamatwa kutokana na mauaji hayo kama haukuwa mpango mpana?
Dhana ya kulipiza kisasi inapungua nguvu kwa kushindwa kusimama kwa miguu miwili. inatuacha njia panda wakati huo ikijaribu kumezwa na dhana mpango wa mapinduzi, kama ilivyodai Serikali.
Inadaiwa kuwa mpango kuipindua, Serikali ya Karume ulibuniwa mwaka 1968 na wanharakati wa mapinduzi ya 1964 wakiwemo raia  na Wanajeshi wachache.
Inasemekana kikao cha mwisho cha mpango huo kilifanyika Aprili 2, 1972 nyumbani kwa Luteni Hamud, ambapo ilikubaliwa kwamba mauaji hayo yafanyike Aprili 7, 1972.
Mpango wa utekelezaji ulikuwa kwamba Hamud na Ahmada wachukue jukumu zito sana la kuiba silaha kutoka Kambi ya Jeshi yaBavuai.

Katika kutekeleza mapinduzi hayo, ambayo mipango na operesheni yake ilifanana kabisa na ya mapinduzi ya 1964, mtu mmoja, Suleiman Sisi, alipewa jukumu la kuongoza mashambulizi kwenye Kambi ya Jeshi la Mtoni na Ahmada alipewa jukumu la Kambi ya Bavuai, Makao Makuu ya Jeshi la Chuo cha Jeshi la Ma­funzo ya Redio ambazo zote ziko eneo la Migombani.

Kambi ya Ubago haikupangi­wa mtekaji kwa kuamini kwamba kama kikosi cha Ahmada kingeweza kuziteka sehemu kili­chopangiwa, Ubago ingesalimu amri sawia.

Kituo cha Polisi Malindi kingetekwa na kikosi ambacho kingeongozwa na Hamud, am­bapo magari yenye redio za mawasiliano yangepatikana kwa watekaji. Ilipangwa kuwa wakati mashambulizi haya yakiendelea, kituo cha Polisi Ziwani kingevamiwa na askari polisi walitarajiwa kuajiriwa na kuongozwa na askari Yusuf Ramadhan.

Mtu mwingine, Amour Dughesh, alipangwa kuteka Ikulu na alipewa jukumu lakumkamata­ Karume na kumpeleka Kituo cha Redio kutangaza kupinduliwa kwa Serikali rake.

Inaelezwa pia kwamba baada ya redio kutekwa, ingewekwa chi­ni ya udhibiti wa Badawi Qual­letein, Miraji Mpatani na Ali Mtendeni. Uwanja wa Ndege ungedhibitiwa na Ali Sultan Issa, ambapo Makao Makuu ya Umoja wa Vi­jana wa AS P (ASPYL) yangetekwa na Baramia.

Makao Makuu ya ASPYL ya­likuwa Kituo Kikuu cha Mkuu wa Usalama wa Ndani ya Serikali ya Karume, Kanali Seif Bakari. Kanali Bakari aliongoza kikun­di cha ukatili kilichojiita kamati ya watu 14, kilichotesa na kuua waliodhaniwa wapinzani na Karume. Abdulrahman Mo­hammed Babu, akiandikia jarida la kila mwezi 'CHANGE' (Vol 4 No. 7,) la 1996, ukurasa 11, anakiri:- "Kutaja pekee jina la Kamati ya Watu 14 kulitosha kumtia mtu woga na kutishika”.

 Kamati hii ili­husika na mauaji ya mamia ya Wazanzibari wasio na hatia, waki­wemo, viongozi, wana’mapinduzi wa kimaendeleo kama Abdallah Kassim Hanga, Abdulaziz Twala, Saleh Saadala, Othman shariff na wengine wale waliuawa kwa jina la Karume."

Abdallah Ameir alipewa jukumu la kuzuia mashambulizi kutoka nje siku hiyo yamapinduzi.
Inadaiwa kuwa katika kikao hicho, Aprili 2, 1972 mtu mmoja, Amar Salim Kuku, alidokeza kuwa Ali Salim Hafidh ambaye nafasi yake haikutajwa katika mpango wa mapinduzi wa Aprili 7, angefi­ka Zanzibar na Abdulrahman Babu na wafuasi wake wa Dar es salaam, usiku wa Aprili 6 kwa mtumbwi kuungana na wanamapinduzi wengine.

Ukiwaondoa Luteni Hamud na Kepteni Ahmada katika mpango huu, na kama ni kweli kwam­ba mpango wote ilikuwa jaribio la mapinduzi (coup d'etat) kama ilivyodai Serikali ya Zanzibar, 'basi staili ya mpango huo haiwezi kut­ofuatishwa na ile ya mapinduzi ya umwagaji damu ya Aprili 12, 1964 ,ambao haukuhusisha jeshi.
Mapinduzi ya 1964 ya kushtukizwa dhidi ya utawala wa Sultan Jamshid na majeshi yake, yali­fanikiwa kwa sababu ya utawala huu kujitenga mbali na wananchi, hivyo haikuweza kupata taarifa za mipango ya mapinduzi hayo mapema.

Na kama ni kweli ilivyosema Serikali ya Zanzibar, kwamba mpango wa mapinduzi ya 1972 uli­buniwa tangu mwaka 1968, ilikuwaje JWTZ na Usalama wa Taifa, achilia mbali kikosi cha Us­alama wa Ndani cha Karume (Gestapo), kilichoongozwa na Kanali Seif Bakari kisibaini mapema hadi siku ya kupoteza uhai wa Kiongozi wa.taifa hilo?  Je, si kweli kwamba historia ya 1964 ilikuwa ikijirudia?

Haya yanaweza kuwa maoni ya wengi, wakiwamo wachunguzi wa mambo ya siasa. Mwanazuoni mahiri barani Afrika, Ali Mazrui anabainisha katika kitabu chake 'Africa's International Relations' (uk. 11); "ukizingatia jinsi Sheikh Abeid Karume alivyoitawala Zanz­ibar kwa ukatili na ubaguzi mkubwa, lolote lilitarajiwa kutokea kwake; hakuna aliyetarajia kwam­ba angedumu kwa miaka minane madarakani. Ndiyo maana hati­maye wengi hawakushangaa alipouawa mwaka 1972."