Monday, June 4, 2012

KATIBA NIITAKAYO

1. SYSTEM OF ELECTION IBADILIKE
hapa Tanzania tumezoa first past the post FPTP ambayo anayeongoza kwa kura anachukua madaraka. kwa mtazamo wangu system hii ya uchaguzi ndiyo inayotufanya tushindwe kupiga kura kwa upande mmoja lakini kwa upande wa pili, inasababisha upotevu wa kura nyingi. kwa mfano Rais Kikwete anaongoza nchi kwa kupata kura 5,276,827 ambayo ukigawanya kwa watanzania miloni 40 ni sawa na aslimia 12.5 ya watanzania wote

lakini pili Dr slaa alipata kura 2,271,941 ambazo ni karibia nusu ya kura Za kikwete, hii  ni kusema zaidi ya watu milioni mbili maoni yao hayajasikilizwa. haiwezekekani watanzania zaidi ya milioni mbili wamchague mtu halafu maoni yao yapotee kwa kuwa wamezidiwa na wengine, kesho hawatapiga kura

katiba mpya ilete system ya propotional Representative ambayo uwakilishi serikalini utatokana na idadi ya asilimia katika kura zilizopigwa. Kwa system hii, hakuna kura itakayopotea kwa maana, hata group dogo la watu kura zao zitapata muwakilishi kwenye serikali hivyo watanzania wataamka kupiga kura

2. MFUMO WA SERIKALI 3
So far tuna mfumo wa serikali mbili, serikali kuu na SMZ, haya ni mapungufu. Zanzibar imeungana na maiti? Tanganyika irudi iwe na serikali yake, Zanzibar iwe na serikali yake na kuwe na serikali kuu ya Tanzania ambayo itakuwa na Rais, makamu, waziri wa ulinzi, mambo ya nje na fedha tu. hii itakata mzizi wa fitina.

3. RAIS ASISHITAKIWE LAKINI, ALIPE MSHAHARA NA POSHO ALIYOPEWA KAMA HAKUTIMIZA AHADI
najua hii itasound kama kichekesho lakini ilani ya uchaguzi ya mgombea husika ni kama business plan, wananchi wanamchagua mgombea flani kutokana na ilani yake, je kama hakutimiza yale aliyosema atafanya, vipi aondoke na mshahara ambao sisi tumempa kwa kazi ambayo hajaifanya.

tumemuona Obama anahaha kuconvince congress lipitishe mambo yaliyo kwenye ilani yake mfano ahadi juu ya bima ya afya, kwa kuwa hiyo ilani ndio iliyompa uongozi

4. JESHI LA WANANCHI NA MAGEREZA YAWE SEHEMU YA KIJAMII NA 25% YA BUDGET YAKE INJITEGEMEE
tufute leseni zote za wakandarasi kutoka nje na kazi za ujenzi wa barabara na kandarasi kubwa ziende kwa jeshi la wananchi. m not suggesting kuwa jeshi halina kazi, lakini lina human resources nyingi za kuweza kufanya kazi za kandarasi na pesa ya ujenzi ikalipe mishahara. natambua kama JKT wanajitahidi kupitia SUMA JKT lakini JWTZ ndio linaloweza zaidi.

kule south Africa wamepiga marufuku gari za kijapan kutembea kwenye ardhi yao labda kwa kibali maalum tangu walivyoamua kutengeneza magari. tuna jeshi lenye watu shupavu, tuna amani, kwa nini mkandarasi wa barabara ya mwenge ubungo awe mchina????

mwengine kaiba kuku wa 15,000 kafungwa miezi sita katumia chakula cha sh 270'000. kwa nini asiambiwe wewe, na wewe, na wewe, mmehukumiwa kupalilia pamba hii mpaka mavuno

5. SHERIA YA KUMLINDA MLAJI
ukinunua gazeti limeandika habari ya uwongo unaruhusiwa kulishtaki na unalipwa fidia, kampuni ya simu imetangaza shilingi kwa sekunde, ikipandisha bei itangaze au ikikata kinyemela ishitakiwe

6. Waziri asiwe mbunge
7. barabara ikitaka kupita kwenye eneo la makazi ya watu, wasilipwe fidia bali serikali ile gharama stahiki za kununua nyumba eneo lile
8. mwananchi ndio mwenye nchi

No comments:

Post a Comment