Thursday, June 28, 2012

LA ULIMBOKA LIWE FUNZO

Hakuna hata mtanzania mmoja ambaye anaweza furahishwa na jambo lililomkuta DR ulimboka, tumuombee mungu amponeshe kwa haraka aendelee simamia lile ambalo yeye anaona ni sahihi

Lakini kubwa zaidi lililonitia hamasa ya kuandika ni wepesi wetu watanzania wa kuhukumu, tunawaachia watoto zetu urithi mbaya sana

Nisieleweke kuwa napingana na kile mnachoamini ninyi bali najaribu kwenda zaidi ya imani yenu.

Vipi Mheshimiwa LEMA angefariki kwa kifo cha kawaida tu kama binadamu wengine ambavyo hufa siku ya pili baada ya kumuandikia waraka rais kikwete? Kwa style yetu ya kuhukumu tungekuwa na amani sisi?

Au Vipi kama mimi nakitaka kiti cha mnyika cha Ubunge na hivyo baada ya drama za "rais dhaifu" nikaamua kumvizia na kumdhuru, nani atanihisi? Najua mtakuwa mshamtaja mhusika bila kunihusisha kabisaaa

Naogopa sana kugusia imani ya wengi juu ya kifo cha sokoine na amina chifupa kwa kuwa itanilazimu niamini na kifo cha chacha wangwe

Nilijaribu soma btn the lines chanzo na matukio ya Rwanda genocide na uhusika wa Ufaransa na kagame, halafu nikasoma utawala wa SIAD BARRE wa somalia, utawala wake, kifo chake na somalia ya leo.

Ikulu ni mahali patamu sana, na wanasiasa wana mbinu nyingi sana za kubaki madarakani au kuingia madarakani Ikibidi hata kwa damu, KENYA ni mfano mzuri... TUJIANGALIE TUNAWEZA GONGANISHWA VICHWA KWA USHAHIDI WA KIMAZINGIRA

Lakini swali la msingi, hawa waliomteka dr ulimboka naskia walikua na bunduki, wamezipata wapi? Kama serikali ingeweka ulinzi wa kutosha tusingeihusisha kirahisi katika mambo kama haya, they should play their part or else kila siku tutaihusisha na kila jambo baya

Anyways ni maoni yangu tu ila mtaani kwetu ukimwambia mtu utanikoma wewe siku ya pili akidhurika polisi wanakubeba, zamu yetu sasa na sisi kuamini kama ambavyo wao huamini yale ya mtaani kwetu

No comments:

Post a Comment