Tuesday, June 5, 2012

TUMETOA DODOKI, TUMEWEKA JIWE LA KUSUGULIA MIGUU

Wakati wa bunge la budget mwaka 2011, mheshimiwa kafulila alimtuhumu Bw Zambi na mbunge mwenzie Omary badwel kwa kuomba rushwa wanapoenda kufanya kazi, akaamriwa kukaa chini

Mheshimiwa felix mkosamali akasimama kuomba muongozo wa mwenyekiti wa bunge ambaye alikuwa mh Simbachawene kwa kuwa tuhuma ni nzito kwa mbunge kuambiwa kaomba rushwa mbele ya bunge tukufu

Mh Simbachawene akasema atalitolea maelezo lakini mpaka leo akalipotezea na hakusema chochote

Leo hii, badwel, mwaka mmoja baadae anakamatwa kwa kosa lile lile la kuomba Rushwa na kufikishwa mahakamani na bw Simbachawene leo hii kapandishwa na kuwa naibu waziri wa nishati na madini.. Usishangae siku akipewa uwaziri kamili wizara hiyo. Wizara yenye kashfa za kutosha..

No comments:

Post a Comment